Tangazo la Kifo – Marehemu Omary Silika



Tangazo la Kifo – Marehemu Omary Silika

Makamu Mkuu wa Chuo anasikitika kutangaza kifo cha Bwana Omary Silika  kilichotokea usiku wa tarehe 15.09.2017 nyumbani kwake Buza.

Kabla ya kifo chake marehemu Omary Silika alikua Muhudumu (Health Attendant) katika kitengo cha Manunuzi (PMU)-MUHAS

Marehemu atazikwa kesho tarehe 17.09.2017 saa kumi (10:00) alasiri huko Buza. Uongozi wa Chuo umeandaa usafiri wa kwenda kwenye msiba na mazishi huko Buza Kanisani. Magari yote yatakuwepo mbele ya jengo la MPL na yataondoka saa tano kamili asubuhi. Tafadhali zingatia muda.

Makamu Mkuu wa Chuo pamoja na jumuia ya MUHAS wanaungana na familia ya marehemu Omary Silika katika kuomboleza msiba huu.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

IMETOLEWA NA:
OFIS YA HABARI NA MAWASILIANO YA UMMA
MUHAS
16/09/2017

See also

HESLB | Higher Education Students Loan Board |

Fisheries Education and Training Agency | FETA |

TCU | Tanzania Commission for Universities |

National Council for Technical Education | NACTE |

Admissions for Universities in Tanzania

Examination Results for Universities in Tanzania

Selected Candidates / Applicants

Necta Examination Results

International Scholarships for Tanzanians to Study Abroad

Sponsored Links

Leave a Comment